Monday 5 February 2018

Okwi afichua siri kuhusu ngumi aliyopigwa na Beki wa Ruvu Shooting.

Image result for Emmanuel Okwi apata maumivu
Mshambuliaji Emmanuel Okwi alipigwa kwenye koo baada ya kupigwa ngumi.
Hali hiyo ilisababisha ashindwe kupumua na kulazimisha mwalimu wake Kocha Pierre Lechantre kulazimika kumpumzisha.

Okwi alipigwa ngumi na beki wa Ruvu Shooting ambaye alitolewa kwa kadi nyekundu.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema mchezaji huyo anaendelea vizuri ingawa alishindwa kupumua baada ya tukio hilo.

“Alipata maumivu baada ya kupigwa ngumi, unajua ngumi ya kisukusuku kwenye koromeo si jambo dogo.

“Lakini tunashukuru anaendelea vizuri na tunatarajia tutakuwa naye kambini maandalizi dhidi ya Azam,” alisema.


Okwi alitolewa baada ya kupigwa kwa makusudi na beki huyo na Ruvu Shooting walicheza kindava wakionekana walikuwa wamepania kuwaumiza wachezaji wa Simba kama ambavyo walicheza kindava katika mechi dhidi ya Yanga ambayo walilala kwa bao 1-0 lakini mshambuliaji Yohana Nkomola naye alitolewa baada ya kuumizwa na hadi sasa ni majeruhi.

USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE





                                SUBSCRIBE ON YOUTUBE 
                                          
                                               TIKISA TV

No comments:

Post a Comment