Tuesday 18 August 2020

YANGA WAFANYA USAJILI MPYA.


 Yanga imeendelea kufanya usajili

wa wachezaji wa ndani na nje ya nchi wakati huu wakirusha 

Jiwe moja na kupiga ndege wawili Tayari viungo wawili (Mukoko

Tonombe na Tuisila Kisinda) kila mmoja amesaini

mkataba wa miaka miwili kujiunga na Yanga

wakitokea AS Vita ya Congo PR.

lakini hadi sasa bado haijulikani kocha wa timu hiyo ni nani.

Ratiba ya Ligi Kuu kwa msimu ujao inatarajia

kuanza mwezi ujao Septemba 6).

Amri Kiemba anasema kunaweza

kukawa na changamoto kwa Yanga kwa sababu klabu

imesajili wachezaji wengi wapya ambao wanakuja

kukutana na benchi jipya la ufundi.

"Kwa namna ambavyo siku zimebaki ili ligi kuanza na

hadi leo timu haina kocha mkuu wala msaidizi, ni

mtihani kwa klabu ya Yanga na vilabu ambavyo hadi

sasa hivi bado havija jua vitakuwa na kocha gani

msimu ujao."

"Kupanga ni kuchagua, haiwezekana kwa namna

ambavyo umechagua kufanya halafu ukategemea

matokeo ambayo yataletwa na kudra na Mwenyezi

Mungu kuliko ambavyo timu imejiandaa.”

"Yanga inawachezaji wengi ambao wameondoka (16)

kuna wachezaji wengi wapya wanakuja sasa

isijekuwa kikundi cha wachezaji badala ya timu."

"Faida kubwa kwa Yanga ingekuwa ni kuwa na kocha

msaidia ambaye alikuwepo kwenye timu msimu

uliopita hata kocha mpya akija anampa ripoti ya

kilichotokea msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment