Wednesday 21 October 2020

Kauli ya Rais Magufuli Vunjo.

 


 Rais John Magufuli ambaye ni Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, amewaasa wananchi wa jimbo la Vunjo kutofanya makosa ya kutompa kura mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Dkt.Charles Kimei, kama wanataka maendeleo ya ukweli.  

Akizungumza na Wanachi wa mji mdogo wa Himo uliopo katika Wilaya ya Moshi vijini, jimbo la Vunjo, Rais Magufuli amesema kuwa Dokta Kimei ni mchapakazi asiye na maneno mengi, lakini amafenya mengi katika nafasi alizohudumu, kuanzia Benki Kuu ya Tanzania na hatimaye Benki ya CRDB. 
 
“Nileteeni Dokta Kimei, huyu Kimei mimi namjua vizuri. Alifanya kazi nzuri Benki Kuu ya Tanzania na akaleta mabadiliko makubwa sana ndani ya Benki ya CRDB pamoja na kusaidia mikoa mbalimbali, ikiwemo Mkoa huu wa Kilimanjaro. Pia amebuni na kusaidia  miradi iliyogusa wananchi wa kawaida. Nitashangaa kama hamtapa kura. Ili tupige hatua za maendeleo, Bunge letu linahitaji watu wa aina ya Dokta Kimei. Nileteeni Kimei” alisema Rais Magufuli.

Akijibu ombi la Dokta Kimei kuhusu kuomba kuanzishwa kwa Wilaya ya Vunjo ambayo itakuwa na Makao Makuu yake katika mji wa mdogo wa Himo, ili kuongeza ufanisi, mapato ya serikali na utawala bora, Rais Magufuli alisema kuwa jambo hili liko ndani ya uwezo wake na kuwasihi wananchi wa Vunjo kumchagua Dkt.Kimei na Madiwani wote 16 ili walisimamie na hatimaye kulifanikisha jambo hilo la msingi.

Kuhusu changamoto ya barabara za kimkakati ikiwemo ile ya Kilema na ya soko la Vunjo. Rais Dokta Magufuli alisaema kuwa suala la ujenzi wa mioundo mbinu liko ndani ya ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na atahakikisha lianfanyiwa kazi haraka iwezekanavyo.

Rais Magufuli anaendelea na ziara yake Mkoani Kilimanjaro ambapo  leo atakuwa na Mkutano mkubwa wa kam

1 comment:

  1. The Casino Junket Club
    Who does the 의정부 출장안마 casino get to 삼척 출장안마 know about? 정읍 출장안마 전라남도 출장마사지 “The casino has a unique atmosphere, and it can run a risk of attracting 여수 출장마사지 new players from around the world.

    ReplyDelete