Sunday 25 October 2015

DK.MAGUFURI KUHITIMISHA KAMPENI ZAKE MWANZA LEO

Jiji la Mwanza naviunga vyake limepata mtikisiko wakati mgombea urais wa chama cha mapinduzi Dr.John Pombe Magufuli alipokuwa akihitimisha kampeni zake za kusaka urais huku rais anayemaliza muda wake Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa ufafanuzi juu ya kuhusika kwake katika sakata la Richmond na kudai kuwa taratibu na kanuni zilikiukwa.
Katika mkutano wa kuhitimisha kampeni za kugombea urais wa chama cha mapinduzi uliohudhuriwa na halaiki ya wakazi wa jiji la Mwanza na viunga vyake kwanza rais Kikwete anatoa onyo kwa wale waliodhamiria kufanya fujo siku ya upigaji kura.
 
Pia Dr.Kikwete anachukua fursa hiyo kukana kuhusika kwake katika sakata la Richmond huku akidai kuwa kanuni na taratibu za kupatikana kwa kampuni hiyo zilikiukwa.
 
Mgombea mwenza wa chama hicho Samia Hassani Suluhu anaueleza umati wa watanzania waliohudhuiria mkutano huo juu ya kero ya upatikanaji wa maji katika maeneo alikozunguka na kuahidi kulipatia ufumbuzi.
 
 
 


 
 
Mgombea wa kiti cha urais Dr.John Pombe Magufuli ambaye amelitikisa jiji la Mwanza na kuvunja rekodi ya mahudhurio katika mkutano huo kwa upande wake ameonesha kukerwa na suala la mgao wa umeme na kuahidi kulitatua na kuto onyo kwa wale wanaohujumu upatikanaji wa umeme.
 
Aidha mbali na kugusia takribani sekta zote kero kwa wananchi pia ameahidi kufufua viwanda vilivyokufa ili kutoa fursa kwa vijana na kuwataka waliobinafsishiwa na kuvitelekeza wanavifufua.
 
Takribani siku 60 za kuomba kura kwa watanzania zimekamilika na sasa wananchi watafanya maamuzi kupitia sanduku la kura kumuweka madarakani kiongozi walioridhishwa na sera zake jumapili ya October 25 ya mwaka huu.

No comments:

Post a Comment