Monday 28 December 2015

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limewataka wananchi kuwa watulivu na kuendelea kulinda amani iliyopo hasa wakati huu wa kuelekea katika sikukuu ya mwaka mpya.



 

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limewataka wananchi kuwa watulivu na kuendelea kulinda amani iliyopo hasa wakati huu wa kuelekea katika sikukuu ya mwaka mpya.
Jeshi hilo limesema   limeweka mikakati   kuhakikisha   wakati wa mkesha wa mwaka mpya   hali ya  usalama inakuwa shwari.
Katika taarifa iliyolewa leo  ambayo imesainiwa na kamishina wa jeshi la  polisi kanda maalum ya Dar es salam Suleimani  Kova imesema jeshi hilo limejipanga vizuri  katika kulinda usalama.

                              Kamanda Suleimani  Kova
Imesema vikosi vyote vya jeshi hilo viko vizuri na pia wana mikakati mbali mbali kwa ajili ya kudumisha amani.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa  kikosi cha anga kitafanya doria kwa kutumia helkopta ya polisi sambamba na  askari wa pikipiki ambao watakuwa na doria katika mitaa mbali mbali.

No comments:

Post a Comment