Monday 28 December 2015

Takwimu nyingine kuhusu Ugonjwa wa kipindu pindu kupungua kwa asilimia kubwa katika mikoa mbali mbali hapa nchini.





Imeelezwa  Ugonjwa wa kipindu pindu umepungua kwa asilimia kubwa katika mikoa mbali mbali hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam waziri wa afya maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto Ummy mwalimu amesema mikoa ya Dar es salaam,mwanza ,Arusha na Mbeya imefanikiwa kwa asilimia kubwa kupunguza kasi ya ugonjwa huo.
 amesema jumla ya mikoa 10, imeathiriwa na ugonjwa wa kipindupindu ambapo kwa sasa  mkoa wa morogoro vijijini,Iramba na Arusha mjini, ndio halmashauri zinazoongoza kwa kuwa na  wagonjwa wengi.
                                                    ummy mwalimu.

 Kufuatia hali hiyo Watendaji wa halmashauri,waganga wakuu na  wilaya wametakiwa kutoa taarifa sahihi za  kila  wiki kuhusu ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment