Tuesday 29 December 2015

MCHEZAJI EL SALVADOR APIGWA RISASI



 
MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa El Salvador, Alfredo Pacheco ameuawa kwa kupigwa risasi. Mtu mwenye silaha anadaiwa kumfuata Pacheco mwenye umri wa miaka 33 na kumfyatulia risasi kadhaa katika kituo cha mafuta kilichopo mji wa Santa Ana kilometa 76 kutoka magharibi mwa mji mkuu wa San Salvador.
 Maofisa wa polisi wamesema watu wengine wawili walijeruhiwa katika tukio hilo ambalo bado wanafanya uchunguzi wa chanzo chake.
 Beki huyo ambaye ndio mchezaji wa aliyeichezea mechi nyingi zaidi nchi yake, alifungiwa maisha kujishughulisha na masuala ya soka mwaka 2013 baada ya kukutwa na hatia ya kupanga matokeo.
 Pacheco na wachezaji wengine 13 wa timu ya taifa walikutwa na hatia ya kupkea rushwa na kupanga matokeo katika mechi kadhaa kati ya mwaka 2010 hadi 2013.
El Salvador, ni Taifa ndogo lililoko Amerika ya Kati, ni moja ya mataifa yenye viwango vya juu zaidi vya mauaji.
Mapema mwezi huu, mchezaji wa timu ya taifa ya Honduras Arnold Peralta, 26, aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa likizoni katika mji wake wa kuzaliwa.

No comments:

Post a Comment