Tuesday 29 December 2015

Mkurugenzi wa huduma za mifugo Tanzania Dk Abdi Haygamo amewatahadharisha wananchi kutojichukulia sheria mkononi ambazo zinasababisha mauaji kwa wakulima na wafugaji.








Mkurugenzi  wa  huduma  za mifugo Tanzania Dk Abdi Haygamo amewatahadharisha  wananchi   kutojichukulia sheria mkononi ambazo   zinasababisha mauaji kwa wakulima na wafugaji.
Kauli hiyo ameitoa  leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusiana na madhara  yatokanayo  na kuchukua sheria mkononi ambapo huleta madhara makubwa katika jamii ikiwemo kiuchumi.
Aidha amesema kuwa Wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi,imepokea kwa masikitiko   mauaji ya wakulima na wafugaji yaliyotokea hivi karibuni   katika wilaya ya mvomero mkoani morogoro  yaliyosababisha  mkulima mmoja kuuwawa,  na watu 4  kujeruhiwa.
Vile vile wizara inatoa pole kwa wote walioathirika  kutokana na mgogoro wa kijiji cha dihida wilayani mvomero mkoani Morogoro.


 

No comments:

Post a Comment