Mhe. Kubenea amesema ni vyema Serikali ikaingilia kati kuondoa utata huo ambao usiposhugulikiwa mapema utaligarimu taifa kutokana na kampuni ya Simon Group kukopa fedha nyingi katika taasisi za kifedha hapa nchini kwa ajili ya kuendesha mradi huo ambao usipofanikiwa utaangusha uchumi wa taifa.
Aidha kubenea ameiomba serikali kuu kuingilia kati sakala hilo ambalo linazidi kuwa na sintofahamau baada ya mchakato wake kugubikwa na udanganyifu mwingi ambao unalipotezea taifa mabilioni ya fedha nakwamba mapendekezo yaliyomo kwenye ripoti ya CAG izingatiwe.
Naye Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita amesema mchakato wa kurudisha vitega uchumi vya mapato ya jiji umefika na kuwa ameunda kamati mbili kuchunguza mradi wa machinga Coplex, kuhakiki makusanyo katika soko la kariakoo, UDA, ikiwa pamoja na kuongeza makusanyo ja jiji kutoka Bilioni 11.7 mpaka bilioni 20 kwa mwaka.
Akiongelea kamati hizo Meya amesema, maeneo muhimu yatakayo angaliwa nipamoja na makusanyo katika soko la Kariakoo, Maduka yanayozunguka eneo la shuke ya Benjamin Mkapa,Machinga Complex, shirika la usafiri la Dar es salaam UDA.
Aidha meya amesema watatumia Bilioni 4 kumaliza kabisa tatizo la Madawati katika shule za jiji la Dar es salaam, na kukarabati barabara ili wananchi wasilalamikie huduma za kijamii sambamba na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano katika ulipaji kodi
No comments:
Post a Comment