Thursday 14 April 2016

Serikali yatoa siku 30 mifugo ya nje ya nchi kuondolewa nchini

 
Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa JUMANNE MAGHEMBE amesema kushuka kwa pato la utalii katika Hifadhi ya taifa ya Ngorongoro kumechangiwa na wafugaji kuingiza mifugo yao ndani ya hifadhi  na kusababisha kushuka kwa hiyo thamani ya wanyamapori na hifadhi.

 Waziri MAGHEMBE amesema hayo katika mahojiano maalumu na Shirika la Utangazaji Tanzania ambapona ametoa siku thelathini kwa mifugo yote toka nje ya nchi kurejeshwa makwao na baada ya muda huo mifugo hiyo itataifishwa na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Waziri MAGHEMBE pia amesema serikali inafanya tathmini ya biashara ya wanyama hai ili kudhibiti usafirishwaji wa wanyama hao kinyume cha sheria.
 Katika hatua nyingine waziri MAGHEMBE amewatahadharisha wafugaji kuepuka kuchanganya mifugo yao na wanyama pori ili kuepuka magonjwa yanayoweza kusambazwa kutoka kwa wanyama pori  kwenda kwa binadamu.
Aidha ameitaka  Wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya wafugaji ili kudhibiti tatizo la uvamizi wa maeneo ya hifadhi

No comments:

Post a Comment