Utafiti umebaini kwamba asilimia 71
ya Watanzania wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35 wanatumia muda wao
mwingi kwenye shughuli zisizo za uzalishaji mali.
Badala yake hutumia muda huo kujihudumia kwenye gesti, baa, kulala na katika shughuli za starehe.
Serikali imesema hali hii inaichelewesha Tanzania kuingia katika kundi la mataifa yenye uchumi wa kati kufikia mwaka 2025.
Bi
Ruth Minja, ambaye ni mtakwimu mkuu katika ofisi ya taifa ya takwimu
Tanzania, ndiye aliyeongoza utafiti huo wa watu wenye uwezo wa kufanya
kazi kwa mwaka 2014/2015.
Anasema waligundua kuwa watu wenye uwezo wa kufanya
kazi walikuwa milioni 25 kutokana na kiashiria cha saa za kufanya kazi
kupungua na baadhi ya wafanyakazi kupunguzwa kazi kutokana na utendaji
dhaifu.
Ally Msaki,
aliyemuwakilisha katibu mkuu katika ofisi ya waziri mkuu
anayeshughulikia masuala ya kazi,vijana ajira na watu wenye ulemavu
amewaangazia Watanzania walioko kwenye ajira, ambao wanapata kipato
ambacho hakitoshelezi kuweza kumudu gharama za maisha.
Amesema nafasi kama hizo za kazi hazina viwango vya ubora na ni kinyume cha maelekezo ya shirika la wafanya kazi duniani ILO.
Ingawa
Sera ya taifa ya ajira kwa Taifa la Tanzania kwa mwaka 2008 ilijikita
zaidi katika kuongeza fursa za ajira na kufanikiwa katika lengo lake,
kuna kasoro kwenye kipengele cha ubora wa ajira.
No comments:
Post a Comment