Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Tamisemi, George Simbachawene akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda nyaraka za jengo la Machinga Complex baada ya kuvunja bodi ya jengo hilo
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -
TAMISEMI GEORGE SIMBACHAWENE ameifuta bodi ya soko la MACHINGA COMPLEX
la jijini DAR ES SALAAM na kuwasimamisha kazi watumishi wanaosimamia
uendeshaji wa soko hilo kwa kushindwa kuwanufaisha wafanyabiashara
wadogo wadogo.
Waziri SIMBACHAWENE ametoa tamko hilo wakati akihutubia mkutano mkuu
wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini uliofanyika jijini DAR ES SALAAM na
kumtaka Mkuu wa mkoa wa DAR ES SALAAM, PAUL MAKONDA kuweka utaratibu
utakaowanufaisha wafanyabiashara wadogo wadogo.
Waziri SIMBACHAWENE amewataka wakuu wa mikoa na wilaya nchini kuwa
walezi wa Jumuiya za wafanyabiashara ili kutatua changamoto
zinazowakabili wafanyabiashara.
No comments:
Post a Comment