Wednesday 20 April 2016

Wajasiriamali wahimizwa kuongeza ubora kwenye bidhaa


Katibu Mtendaji Mamlaka ya Leseni ZANZIBAR RASHID ALI SALUM amesema endapo wajasiriamali wataweza kuzingatia uzalishaji wa ubora wa bidhaa basi kunauwezekano mkubwa wa kupata masoko ya uhakika nje ya nchi
Akizungumza na wajasiriamali katika semina mjini Unguja inayohusu masuala ya kuboresha bidhaa katika kiwango cha kimataifa

Amesema licha ya  kuweko kwa changamoto za uzalishaji wa ubora wa bidhaa lakini bado kunahaja  ya kuhakikisha  bidhaa zinazozalishwa zinakidhi mahitaji ya ndani na nje ya nchi

Naye  Kaimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa  na Maendeleo ya Viwanda UNIDO GERALD RUNYORO amesema katika ushindani huo wa kibiashara wajasiriamali wanapaswa kuzingatia ubora na ufungaji uwe katika muonekano mzuri na kuzingatia sheria za usajili wa bidhaa.

Semina hiyo imejumuisha wajasiriamali wa bidhaa za usindikaji, za kutengeneza kwa mikono, biashara ndogondogo na utalii kutoka Unguja  na PEMBA.

No comments:

Post a Comment