Thursday 12 May 2016

Hans-Pope atoa kauli hii kuhusu klabu ya Simba SC kutofanya vizuri.






Hans pope amesema, kwa upande wa mechi za Simba na Yanga haziangalii ubora wa timu kwani zinamambo yake mengi sana na wao kama Simba walijiamini kuchukua ubingwa kutokana na mwenendo wa timu ulivyokuwa tangu mwanzo wa Ligi.

Pope amesema, kufanya vibaya kwa timu kumeanza katika mchezo wa Robo fainali ya Kombe la Shirikisho Tanzania Bara waliyocheza dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam suala lililoonyesha moja kwa moja kuwa kunajambo ambalo lipo ndani ya timu na kuifanya timu kuwa hivyo.

Pope amesema, anaamini kunawatu wanawashika wachezaji ili wacheze chini ya kiwango na matokeo yake wanashindwa kushindwa mechi mbalimbali hivyo wanalifanyia uchunguzi jambo hilo ili kujua ni watu gani na wanafanya hivyo kwa sababu gani.

Pope amesema, ilionekana dhahiri wanauwezo wa kuchukua ubingwa wa msimu huu lakini walipofika katika hatua nzuri ya kuwania ubingwa wa msimu huu ndipo pale kiwango cha baadhi ya wachezaji kilipoanza kushuka.

Pope amesema, kwenye siasa za Simba na Yanga fujo huanza pale mashabiki wanapotaka kumtoa kiongozi na uongozi ukishatoka huwa wanakuwa na mtu wao wanataka aingie.

Pope amesema, fujo za safari hii zimeandaliwa kabisa na baadhi ya watu kwani imefikia hatua mpaka baadhi ya wachezaji kupiga wachezaji wenzao kwa sababu wanajua kilichofanyika katika mchezo dhidi ya Toto ambapo Simba ilipoteza kwa bao 1-0 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Pope amesema, mashabiki wanatakiwa kuangalia timu na wachezaji wanachokifanya na sio kushambulia viongozi kwani wachezaji ndio chanzo na kama wangewafuata na kuwaambia wangeweza kubadilika katika mechi zinazofuata.

Kwa upande mwingine Hans Pope amesema, kwa upande wa wachezaji kugoma wakishinikiza kulipwa mishahara yao sio sahihi kwani wanajua kabisa muda wa kulipwa mshahara ni kati ya tarehe tano au 10 sasa suala la kugoma kati ya tarehe sita na saba inaonekana ni msukumo kabisa.

Pope amesema, mshahara mara zote inatoka kwa wadhamini kwani wadhamini watatoa pesa wiki ya kwanza ya mwisho wa mwezi au wiki ya pili hivyo inaonekana kugoma kwa wachezaji ni shinikizo kutoka kwa baadhi ya mashabiki ambao hawana nia nzuri na timu hiyo.

Pope amesema, msimu huu walikuwa na timu bora kuliko misimu yote ambayo ineweza kuchukua Ubingwa lakini anaamini mashabiki wasio na nia nzuri na timu ndio chanzo cha kuiharibu timu mpaka imefikia hatua iliyopo sasa.

Simba imesaliwa na michezo miwili ikiwa na pointi 59 huku ikiendelea kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.

No comments:

Post a Comment