Sunday 15 May 2016

Vifahamu vyakula na vinywaji vinavyosababisha Magonjwa ya saratani kwa binadamu.

 
Tafiti zinaonesha kwamba asilimia kubwa ya  magonjwa ya saratani kwa binadamu  husababishwa na matumizi ya chakula au vinywaji ambavyo vina mabaki ya chembechembe za mionzi  ya nishati ya nyuklia ambayo ilitupwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo baharini na maeneo ya jirani baada ya mlipuko wa  kinu cha  nguvu za nyuklia cha Chernobyl nchini Ukraine miaka 30 iliyopita.

Kufuatia  Mkasa huo  ambao unatajwa kuacha sumu ya kudumu itokanayo na chembechembe za  mionzi ya nyuklia katika maeneo mbalimbali ,Shirika la nguvu za atomic duniani liliweka utaratibu wa kuhakikisha vyakula vyote vitokanavyo na  nafaka ,nyama na vinywaji  vinapimwa kabla ya matumizi yake ,shabaha ikiwa ni kubaini uwepo wa  mabaki ya mionzi ya nyuklia au laa. ambapo kwa Tanzania jukumu hilo liko chini ya tume ya nguvu za atomic

Ni katika jumba hili ambalo ndipo sampuli za shehena  zote za vyakula,sukari,mafuta ya kupikia, vinywaji na mbolea  kutoka nje na sehemu nyingine ambazo hutiliwa shaka  hufikishwa hapa na kufanyiwa vipimo vya kimaabara  ili kulinda afya za walaji.

Mkurugenzi mkuu wa Tume ya nguvu za atomi nchini yenye makao yake makuu jijini  hapa anawatoa wasiwasi waagizaji wa bidhaa zote ambazo zinatiliwa shaka kwa kuwa na uwezekano wa kuwa na mabaki ya mionzi ya nyuklia

No comments:

Post a Comment