Tuesday, 11 October 2016

TFF yatoa msimamo huu kuhusu suala la klabu ya yanga kukodishwa.

Image result for Celestine Mwesigwa
Shirikisho la soka nchini TFF, limetoa 
msimamo wake kuhusu suala la klabu ya 
Yanga kukodishwa kwa muda wa miaka kumi 
kwa kampuni ya Yanga Yetu.


Katika mkutano na waandishi wa habari 
uliofanyika mapema hii leo, katibu mkuu wa 
TFF Celestine Mwesigwa amesema shirikisho 
halijapata taarifa yoyote kuhusiana na 
mabadiliko yoyote katika klabu ya Yanga 
licha 
ya kusoma taarifa hizo katika vyombo vya 
habari.

Mwesigwa amesema TFF bado inatambua 
hadhi ya Yanga kubaki vilevile hadi 
watakapopewa taarifa rasmi na uongozi wa 
klabu hiyo na kuzipitia ili kuhakikisha kama 
kanuni na taratibu za TFF, CAF na FIFA 
zimefuatwa.

‘Nimewaandikia klabu ya Yanga watupe 
nakala za mkataba wa ukodishwaji 
watuelezee nini kimeuzwa, kipi 
kimekodishwa. Kwa sasa msimamo wa TFF 
ni kuwa hadhi ya Yanga iko pale pale.’

TFF wametangaza msimamo huo ikiwa ni 
siku kadhaa baada ya baraza la michezo la 
taifa BMT, kuwataka Yanga kufuata taratibu 
za kikatiba ili kukamilisha mchakato ambao 
umedhamiriwa kufanywa kupitia bodi ya 
wadhamini na uongozi wa kampuni ya Yanga 
Yetu ambayo ipo chini ya mwenyekiti Yusuf 
Manji.

Katibu mkuu wa BMT Mohamed Kiganja, 
alieleza wazi kuwa mchakato wa kukodishwa 
kwa klabu ya Yanga ni batili kutokana na 
suala hilo kutokuwa na baraka za mkutano 
mkuu wa wanachama na pia bodi ya 
wadhamini ambayo inadaiwa kusaini 
mkataba 
wa kukodishwa aliita kuwa ni batili kufuatia 
kuwa na wajumbe wasiotambulika kisheria.

USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE

No comments:

Post a Comment