Wednesday 9 November 2016

VIDEO:Alichokizungumza Hillary Clinton baada ya kushindwa na mpinzani wake Donald Trump.

Image result for hillary clinton
Mgombea wa urais aliyeshindwa katika uchaguzi mkuu wa Marekani Hillary Clinton amesema kuwa rais mteule Donald Trump anafaa kupewa nafasi ili kuongoza.

Akionekana kwa mara ya kwanza tangu kukiri kushindwa ,mgombea huyo wa chama cha Democrat amesema kuwa ana matumaini kwamba Trump atafanikiwa kuwa rais wa Wamarekani wote.
''Tumeona kwamba taifa letu limegawanyika sana zaidi ya nilivyodhania'',alisema bi Clinton.
Donald Trump atakuwa rais wa 45 wa Marekani baada ya ushindi mkubwa.



Bi Clinton aliwaambia wafuasi wake akitaja kushindwa kwake katika uchaguzi huo katika hotubu yake huko New York.
''Bado hatujaafikia lengo letu .Lakini siku moja mtu ataafikia'', alisema Bi Clinton.
''Kwa wasichana wote wanaotazama hotuba hii...ondoeni shaka kwamba muna thamani tele na uwezo mkubwa na munapaswa kupewa kila fursa duniani'',alisema. Nawapa pole kwamba hatukushinda kutokana na thamani tulio nayo kati yetu na maono yetu tulionayo kwa taifa hili''.


USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE

                              SUBSCRIBE ON YOUTUBE TIKISA TV

No comments:

Post a Comment