Wednesday 30 November 2016

Waziri Nape Nnauye atoa maamuzi kuhusu mgogoro wa pambano la Dullah Mbabe na Francis Cheka.

Image result for nape nnauye
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye, amefanikiwa kumaliza mgogoro uliozua hofu ya kutokuwepo kwa pambano la Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ na Francis Cheka lililopangwa kufanyika Desemba 25, mwaka huu kwenye Ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar.

Kutokana na kuwepo kwa mgogoro huo, iliwalazimu viongozi wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), kutinga kwenye ofisi za Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kumaliza mgogoro huo kama walivyotakiwa kufanya hivyo na Nape.

Kaike Siraju ambaye ni promota wa pambano hilo, 
amesema: “Tunamshukuru Waziri Nape kwa kusimamia mgogoro huu na kuumaliza kabisa, sasa pambano lipo palepale kama lilivyopangwa, hivyo tunawashukuru wote walioshiriki katika kupigania kumaliza tofauti zilizojitokeza.


“Mashabiki wa masumbwi popote walipo wasiwe na wasiwasi, Desemba 25 waje pale PTA kushuhudia pambano hilo kali na tayari nimepata taarifa kwamba mabondia wote wanajifua vikali kila mmoja akitaka kumshinda mwenzake.

USISAHAU KULIKE NA KU-SHARE NA KU-LIKE PAGE YETU FACEBOOK TIKISA MEDIA KUFOLLOW TWITTER @TIKISA MEDIA NA INSTAGRAM TIKISA ENTERTAINMENT MEDIA ILI HABARI ZOTE KUBWA ZIKUFIKIE HAPO ULIPO.ASANTE



                                SUBSCRIBE ON YOUTUBE 
                                          
                                               TIKISA TV

No comments:

Post a Comment