Friday 8 December 2017

Anna Mgwhira atoa sababu ya kuamia rasmi CCM.

Image result for Anna Mgwhira
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa ACT Wazalendo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwhira ametangaza kukihama chama hicho na kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Ijumaa, Desemba 8, 2017 baada ya kueleza kuwa ameridhishwa nayo.


Mghwira amejiunga na CCM baada kukakiribishwa na Rais Magufuli kuzungmza na kuwasalimia wananchama katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake CCM(UWT) ambapo amesema ameona si vibaya kujiunga na CCM.

“Kutokana na kazi niliyofanya na serikali kwa kipindi cha miezi sita, nimependa kwa utaratibu mnaofanya katika utaratibu wa vikao, ni jambo jema kwa chama na kwa jami.

Ninaiona CCM inayobadilika katika mkoa ninaouongoza kwa kuanza kukataa rushwa, sioni kama kuna mtu anayetaka kubaki, kwa machache hayo napenda kutamka kwamba naungana na CCM,” amesema Mghwira.

No comments:

Post a Comment