Tuesday 23 January 2018

Kamanda Simoni Sirro Uso kwa Uso na Nabii Tito Dodoma.

JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma inadaiwa limemtia mbaroni mkazi mmoja wa mkoani humo anayejitangaza kama nabii, Tito Machija, ambaye amekuwa akionekana mitandaoni akifanya mambo yasiyoendana na maadili ya dini na injili anayodai kuihubiri.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro,  amezungumza na ‘mhubiri binafsi’ huyo licha ya jeshi hilo kutotoa taarifa rasmi ya kilichojiri na utaratibu unaoendelea iwapo ni kumhoji au kumfikisha mahakamani.

Nabii huyo ambaye video zake zimesambaa akihamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, ikiwa ni pamoja na kutembea na wafanyakazi wa ndani,  anatumia pombe kunasa waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, ambazo nyingi hufanyikia baa.

Aidha ameonekana akicheza nyimbo za Bongo Fleva akiwa ‘madhabahuni’ badala ya kwaya na huku akieleza kuwa wafadhili wake wanatumia pombe,  hivyo na yeye lazima waumini wake watumie pombe ambazo amezifanyia upako.

No comments:

Post a Comment