Saturday 17 February 2018

Salum Mwalimu atoa msimamo wake kuhusu kinachoendelea katika uchaguzi wa kinondoni.

Image result for Salum Mwalimu Uchaguzi
MGOMBEA Ubunge wa jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), amesema yupo tayari kuitwa mhalifu ama kupelekwa jela yeyote iwapo ataonekana ametenda kosa kutetea kura zake.


Salum ameyasema hayo leo kufuatia baadhi ya mawakala wa uchaguzi wa chama hicho kuzuiliwa kuingia kwenye vituo na baadhi yao waliokuwa wameingia wametolewa kwa sababu wanatakiwa kuwa na barua ya utambulisho wa wakala kutoka Tume ya Uchaguzi NEC. 

Salum amelalamikia suala la mawakala wa Chadema kutolewa katika vyumba vya kupigia kura, huku akionyesha wazi kutoridhishwa na utendaji kazi wa baadhi ya polisi waliotanda katika vituo vya kupigia kura, na kusema ana hofu huenda miongoni mwa askari hao kuna wengine ni askari feki.


No comments:

Post a Comment