Thursday 20 February 2020

Tetesi zote za Soka kutoka Ulaya Alhamisi 20.02.2020



Mshambuliaji wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi, 32, amepigiwa simu na klabu ya LA Galaxy kujadili uhamisho wa kuelekea Ligi ya Soka ya Marekani (MLS). (Express)

Messi amekiri kuwa anahisi kuna "mambo ya ajabu" yanaendelea Barcelona huku kukiwa na ripoti kuwa klabu hiyo ilikodi kampuni ya mitandao ya kijamii kukashifu wachezaji wake. (Mundo Deportivo, via Mail)
Hata hivyo, Messi yungali anaiona Barcelona kama nyumbani kwake licha ya tetesi za kutaka kuihama klabu hiyo. (ESPN)


Klabu ya Manchester United inaimani kuwa itamnasa mshambuliaji wa klabu ya Borussia Dortmund na timu ya taifa ya England Jadon Sancho, 19, mwishoni mwa msimu, lakini kwanza itawapasa kufuzu kwa mashindano ya Klabu Bingwa Ulaya. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa RB Leipzig Timo Werner, 23, amesema kuwa anajisikia fahari kuhusishwa na klabu ya Liverpoollakini anahisi kuwa huenda hayupo tayari kujiunga na klabu hiyo ambayo anasema ni "timu nzuri zaidi duniani." (Metro)


Klabu ya Juventus imewaorodhesha mshambuliaji wa Manchester City na Brazil Gabriel Jesus (22) pamoja na mshambuliaji wa Paris St-Germain na Argentina Mauro Icardi (27) kama kipaumbele katika dirisha l usajili la mwishoni mwa msimu. (Tuttosport - in Italian)
Mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud, 33, amesisitiza kuwa atacheza kwa moyo wote kwa Chelsea licha ya kushindwa kuihama klabu hiyo katika dirisha la usajili la mwezi uliopita. (Mirror)


Klabu ya Arsenal inamnyatia beki wa Bayer Leverkusen Jonathan Tah, 24, ambaye anaweza kuondoka katika klabu yake kwa dau la euro milioni 40 mwishoni mwa msimu. (Bild - in German)

Kiungo wa Leverkusen na timu ya taifa ya Ujerumani Kai Havertz, ambaye anahusishwa na tetesi za kuhamia Liverpool, anaweza kuruhusiwa kuihama klabu yake mwishoni mwa msimu, amedokeza mkurugenzi wa ufundi wa klabu hiyo. (Goal)

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta amekiri kuwa hakumpanga kiungo Matteo Guendouzi, 20, katika mchezo dhidi ya Newcastle kutokana na utovu wa nidhamu walipokuwa katika mapumziko Dubai hivi karibuni. (Mirror)

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba anatarajiwa kuondoka Manchester United msimu huu lakini klabu hiyo inataka zaidi ya £150m kumuachilia mchezaji huyo wa miaka 26. (ESPN)

 
Wakala wa Pogba, Mino Raiola anasema kuwa ana mpango wa "kuwasiliana" na mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer baada ya majibizano makali kumhusu mteja wake. (Sky Sports)


Manchester City inamtaka winga wa Bayern Munich Serge Gnabry, 24, kama sehemu ya mpango utakaomwezesha Leroy Sane, 24, kujiunga na klabu hiyo ya Bundesliga. (Sun)



Mkufunzi wa Chelsea Frank Lampard ataelekezewa darubini kali ikiwa klabu hiyo itashindwa kufuzu kwa Champions League msimu huu. (Telegraph)


Manchester City huenda ikakabiliwa na uchunguzi zaidi kutoka Uefa ili kubaini kiwango cha wafadhili wake wa Abu Dhabi baada ya kuwekewa marufuku ya kushiriki mashindano ya ulaya baada ya kupatikana na kosa la kiuka sheria ya uchezaji haki kifedha. (Guardian)

No comments:

Post a Comment