Wednesday 26 February 2020

Virusi vya Corona vyaingia nchini Algeria.

 
Waziri wa Afya nchini Algeria amethibitisha kwamba nchi hiyo imepokea kisa cha kwanza cha coronavirus katika taarifa iliyotolewa na runinga inayomilikuwa na serikali, ENTV Jumanne jioni.


Waziri Abdel Rahman Ben Bouzid alisema kuwa mgonjwa huyo ni mwanamume raia wa Italia aliyewasili nchini humo Februari 17, kulingana na shirika la habari la Reuters.
Mgonjwa huyo ametengwa kwa sasa. 

Algeria imekuwa nchi ya pili Afrika kuthibitisha kupata mgonjwa wa virusi vya Corona.
Misri ilikuwa ya kwanza kuthibitisha kupatika kwa kisa cha virusi vya Corona lakini baadae ikatangaza kwamba mgonjwa huyo hana tena maambukizi na anaendelea kupata nafuu. 


.Wakati huo huo, naibu waziri wa afya na mbunge mmoja nchini Iran wamethibitishwa kupata virusi vipya vya Corona, wakati inapambana kukabiliana na virusi hivyo ambavyo vimesababisha vifo vya watu 15. 

Watu wengi zaidi wamefariki nnchini Iran kwasababu ya virusi hivyo kuliko nchi nyengine yoyote mbali na China. 

Nchi hizo mbili zina uhusiano mkubwa wa kibiashara.

Nchi zingine ambazo kwa sasa zimekumbwa na mlipuko wa virusi vya Corona kwa kiwango kikubwa ni Korea Kusini na Italia ambapo visa hivyo vimekuwa vikiongezeka katika siku za hivi karibuni. 

 
☆Unaitaji kununua nyumba,Gari,viwanja au kupangisha nyumba ,kuuza nyumba ,magari ,Viwanja
☆Hunaitaji Frem Bora ya kifanyia Biashara
☆Hunatafuta nyumba za kupanga kwa gharama nafuu?
Basi  Huitaji kupata shida jibu ni moja tu @dalalinyota ndio mtatuzi wa mahitaji yako yote.
Kwa Nyumba Bora ,Frem za Bora za Biashara ,Viwanja,Nyumba za kupanga,kuuza/kununua Nyumba,Magari,viwanja
Wasiliana na Dalali Muaminifu mjini
FOLLOW @dalalinyota @dalalinyota
PIGA 0758306396
           0654412744.

No comments:

Post a Comment