Wednesday 26 February 2020

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 26.02.2020

 
Manchester United inaweza kuwauza mshambuliaji wa England Jesse Lingard, 27, na kiungo wa Brazil Andreas Pereira, 24, mwishoni mwa msimu. (Express)


United wameongeza kasi katika mpango wao wa kutaka kumsajili kiungo na nahodha wa Aston Villa Jack Grealish, 24. (Manchester Evening News)

Arsenal inaweza kupokea ofa za usajili wa mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang 30. Mkataba wake na Arsenal unamalizika mwakani. (Mail)


Hata hivyo, mshambuliaji huyo wa Gabon bado hajasema kuwa hatasaini mkataba mpya na Arsenal japo mazungumzo na klabu yamedumaa. (Metro)

Rais wa klabu ya Juventus Andrea Agnelli amesema klabu inataka kumchukua kocha wa Manchester City Pep Guardiola. (Manchester Evening News)


Barcelona watatakiwa kuilipa Liverpool pauni milioni 225 ili kumsajili winga Msenegali Sadio Mane, 27.(Mirror)

Manchester City ipo hatarini kuwapoteza baadhi ya wachezaji wake nyota, akiwemo mshambuliaji wa England Raheem Sterling, 25, endapo watatwaa ubingwa wa if they win Champions League msimu huu. (ESPN)


Beki wa Real Madrid Sergio Ramos, 33, hana haraka ya kuingia katika mazungumzo ya mkataba mpya huku akisema mahusiano yake na Madrid ni mazuri.(Goal)

Kocha wa timu ya taifa ya UhispaniaLuis Enrique ameingia mashaka juu ya kiwango cha kipa wa Chelsea Kepa Arrizabalaga, 25, kuelekea kwenye Kombe la Mataifa ya Ulaya kwa kutopata muda mwingi wa kucheza. (AS - in Spanish)

Winga wa England Jadon Sancho, 19, anaweza kusalia na Dortmund baada ya msimu huu ingawa alikuwa akihusishwa na taarifa za kuhamia Chelsea, Liverpool au Manchester United. (Ruhr Nachrichten - in German)

Leicester City inafikiri kumpatia mkataba mpya Christian Fuchs, 33, wakati mchezaji huyo wa nafasi ya ulinzi akikaribia kumaliza mkataba wake. (Mail)


Kiungo wa kati wa Manchester United Nemanja Matic, 31, anatarajiwa kuondoka wakati mkataba wake utakapokwisha mwishoni mwa msimu huu, huku mawakala wakiendelea kutathimini timu, lakini AC Milan hawana mpango wa kumsajili kutokana na matakwa yake ya mshahara. (Calciomercato)

Kiungo wa kati wa Arsenal Granit Xhaka, 27, amesema anahofia hataichezea klabu hiyo tena baada ya kupoteza unahodha wake.(Evening Standard)

 Roma na Manchester United wamebaki kwenye mazungumzo kuhusu mchezaji wa nafasi ya ulinzi Chris Smalling, 30, na mpango wa kuhamia Italia kwa mkataba wa kudumu. (Star)

 
☆Unaitaji kununua nyumba,Gari,viwanja au kupangisha nyumba ,kuuza nyumba ,magari ,Viwanja
☆Hunaitaji Frem Bora ya kifanyia Biashara
☆Hunatafuta nyumba za kupanga kwa gharama nafuu?
Basi  Huitaji kupata shida jibu ni moja tu @dalalinyota ndio mtatuzi wa mahitaji yako yote.
Kwa Nyumba Bora ,Frem za Bora za Biashara ,Viwanja,Nyumba za kupanga,kuuza/kununua Nyumba,Magari,viwanja
Wasiliana na Dalali Muaminifu mjini
FOLLOW @dalalinyota @dalalinyota
PIGA 0758306396
           0654412744.

No comments:

Post a Comment