Monday 2 March 2020

Kauli ya Katibu wa CCM Bashiru kuhusu Benard Membe

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt Bashiru Ally, amemuomba aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, aache kutapatapa na kwamba anahitaji kufanyiwa ushauri wa kisaikolojia ili aweze kuwa sawa.


Dr Bashiru Ameyasema hayo wakati akizungumza  katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi leo tarehe 2 Machi 2020 jijini Dar es Salaam

Amesema CCM wamechukua hatua hiyo baada ya hatua za awali kushindwa kufanikiwa....
"Ndugu Membe alishawahi kupewa adhabu ya onyo kali ikiwa ni hatua ya kujaribu kumpa nafasi ya kujirekebisha, lakini ilishindikana,  huu ni uamuzi mgumu tuliochukua, na si kusherehekea na nisingependa WanaCCM kujitokeza hadharani kufurahia.
" Nadhani tumpe muda, ni binadamu ana haki zake,  anahitaji ushauri nasaha, maana siyo tatizo dogo hili na mimi sitaki kulizungumza kwa ushabiki hata lingenipata mimi ningehitaji marafiki zangu wa karibu niwashirikishe" amesema Dkt Bashiru.
 

Dk. Bashiru ameeleza kuwa, milango ya CCM  kupokea wanachama wanaokiri makosa yao na kuomba msamaha iko wazi, hivyo Membe anaweza kukata rufaa juu ya suala hilo.

“Mchakato huu ni kama wa kimahakama kuna rufaa, nikianza mimi kusema wakati mimi ndio nitapokea rufaa kama nipo ni kama naingilia mchakato wa haki. Na matarajio yangu ni kwamba atarudi CCM, nikiwa hai au nimekufa.

“Sababu milango ya kuwapokea wanachama iko wazi na kuondoka iko wazi, mimi nimesaini barua za misamaha 14 na niko tayari kusaini ya 15 ambayo ni ya Membe kurudi kama akitaka,” amesema Dk. Bashiru.
 
 ☆Unaitaji kununua nyumba,Gari,viwanja au kupangisha nyumba ,kuuza nyumba ,magari ,Viwanja
☆Hunaitaji Frem Bora ya kifanyia Biashara
☆Hunatafuta nyumba za kupanga kwa gharama nafuu?
Basi  Huitaji kupata shida jibu ni moja tu @dalalinyota ndio mtatuzi wa mahitaji yako yote.
Kwa Nyumba Bora ,Frem za Bora za Biashara ,Viwanja,Nyumba za kupanga,kuuza/kununua Nyumba,Magari,viwanja
Wasiliana na Dalali Muaminifu mjini
FOLLOW @dalalinyota @dalalinyota
PIGA 0758306396
           0654412744.

No comments:

Post a Comment