Friday 27 November 2015

Liverpool yatamba katika ligi ya Europa(+picha) Jurgen atowa ya moyoni

 Liverpool striker Christian Benteke celebrates his goal during his side's 2-1 Europa League victory against Bordeaux
          Mshambuliaji wa liverpool Christian Benteke
The Liverpool players celebrate Benteke's brilliant solo strike as they take a 2-1 lead just before half-time 

Michuano ya Europa Ligi imeendelea tena jana kwa michezo mbalimbali katika hatua ya mtoano.
Miongoni mwa mechi zilizochezwa ni Liverpool dhidi ya Bordeaux ambapo Liverpool imechomoza na ushindi wa bao 2-1 mabao ambayo yamefungwa na James Milner pamoja na Christian Benteke.
Tottenham imeichapa Qarabag bao 1-0, Schalke 04 imeifunga Apoel Nicocia bao 1 – 0 , Monaco imechapwa bao 2-0 na Anderlecht.
FC Augsburg imelala bao 3-2 dhidi ya Athletic Bilbao, Ajax imeifunga Celtic bao 2-1 na FK Krasnodar imeiadhibu Borussia Dortmond bao 1-0.
Michuano hiyo itaendelea tena December 10 kwa michezo kadhaa, ikiwemo Fenerbahçe itaikabili Celtic, Tottenham watakuwa wenyeji wa Monaco, FC Sion itaikaribisha Liverpool.
 Klopp celebrates at full-time at Anfield with goalkeeper Simon Mignolet despite his blunder that offered Bordeaux a chance to take the lead

No comments:

Post a Comment