Thursday 26 November 2015

Manispaa ya Ilala yafanya zoezi la kupunguza Omba Omba

Halmashauri ya Manispaa ya ILALA kupitia Idara ya Mendeleo ya Jamii na vijana imefanya zoezi maalum la kuondoa ombaomba katika manispaa hiyo kuanzia tarehe 30 ya mwezi uliopita.

Akizungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo na ustawi wa jamii wa Manispaa hiyo Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ISAYA MUNGURUMI amesema zoezi hilo litakuwa endelevu ili kuhakikisha kwamba linakwisha kabisa na usafi wa jiji wa DSM unadumishwa.

MUNGURUMI amesema sheria zimeshaanza kutumika kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani ombaomba wanaozurura mitaani mchana na usiku na kuwatumikisha watoto kinyume cha sheria.
Amebainisha kwamba wazazi wanapaswa kushitakiwa kwa kuvunja sheria ya kutowapa watoto haki zao za msingi pamoja na ulinzi na kuwafanyisha kazi kinyume cha taratibu katika mazingira hatarishi na ya udhalilishwaji.
Aidha Halmashauri hiyo imeunda kikosi kazi kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo kinachojumuisha wadau wa sekta mbalimbali zikiwemo

No comments:

Post a Comment