Wednesday 11 November 2015

Rais wa marekani Barack Obama ajiunga na mtandao wa Facebook

 
Rais wa Marekani Barack Obama hatimaye amejiunga na Facebook, na ujumbe wake wa kwanza umekuwa ni wa kuhimiza watu kuchukua hatua kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Ikulu ya White House kwenye ukurasa huo wake imepakia video ya Obama akitembea katika eneo la South Lawn katika ikulu ya White House.
 

 Hatua yake ya kujiunga na Facebook, mtandao wa kijamii wenye zaidi ya watumiaji bilioni moja, inaonekana kama juhudi za kiongozi huyo kuwafikia zaidi vijana na makundi mbalimbali ya watu.
“Natumai mtachukulia huu kuwa ukumbi ambao tunaweza kutumia kujadiliana kuhusu masuala muhimu kuhusu taifa letu,” anasema kwenye video hiyo.
Obama anaonekana akitembea kwenye bustani hiyo ambayo imekuwa chini yake kwa miaka saba iliyopita, ambayo kama anavyosimulia, ina mbweha, mwewe na vichakuro.
Lengo kuu la kisiasa hata hivyo linaonekana kuhimiza ulimwengu kuunga mkono juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

No comments:

Post a Comment