Friday 18 December 2015

Kikosi cha makomando wa nchini Marekani kilichoenda nchini Libya siku chache zilizopita kwa ajili ya kuimarisha uhusiano



 
Kikosi cha makomando wa nchini  Marekani kilichoenda nchini Libya siku chache zilizopita kwa ajili ya kuimarisha uhusiano na mawasiliano na jeshi la nchi hiyo kimetakiwa kutoka nchini humo.
 Afisa wa Wizara ya Ulinzi nchini  Marekani  ambaye hakutaka jina lake litajwe amethibitisha kuwa, picha zilizosambazwa katika mitandao ya  kijamii  na jeshi la Libya zikionyesha makomando hao  wakiondoka nchini humo, ni za kweli.
Makomando wa Marekani wadhalilishwa nchini Libya
Amesema makomando hao walilazimika kuondoka Libya muda mfupi baada ya kuwasili, baada ya kutakiwa kufanya hivyo na kundi moja la waasi katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
Kikosi hicho cha makomando wa Marekani kilienda Libya mnamo Disemba 14, kwa kile kilichotajwa kuwa ‘kuimarisha uhusiano wa kiulinzi na kiusalama na jeshi la nchi hiyo

No comments:

Post a Comment