Friday 18 December 2015

Muungano wa Afrika umetangaza mpango wa kutuma walinda amani nchini Burundi ili kuzuia machafuko zaidi.



 
Muungano wa Afrika umetangaza mpango wa kutuma walinda amani nchini Burundi ili  kuzuia machafuko zaidi.
Uamuzi huo umetolewa wiki iliyopita katika mkutano uliofanyika nchini Addis Ababa Ethiopia.
Umoja wa Mataifa unakadiria watu zaidi ya mia nne  wameuawa tangu kuanza kwa  machafuko hayo  mwezi Aprili wakati  Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwania tena  nafasi ya  urais kwa muhula wa tatu.
Maafisa wa UN wameonya  nchi hiyo kukabiliwa na hatari ya kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Lakini mauaji mabaya zaidi yametokea Ijumaa ya  wiki iliyopita wapiganaji waliposhambulia maeneo ya jeshi Bujumbura na kusababisha watu 87 kupoteza maisha.


No comments:

Post a Comment