Thursday 21 April 2016

Wa-shia wasema haya juu ya serikali ya Magufuli.

 
Kiongozi Mwandamizi wa dhehebu la Kiislamu la Shia Ithnashery nchini Tanzania Imamu Swadiq Sheikh Hemed Jalala ameitaka Serikali ya awamu ya tano kuzingatia utawala bora na kuweka usawa baina ya wananchi bila ya kuangalia tofauti zao ili kwa pamoja waeze kujiletea maendeleo.

Sheikh Jalala ameitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mrithi wa Mtume Muhamad Imam Ali ambae alikufa miaka elfu moja na 30 iliyopita lakini anakumbukwa kwa utawala wake wa kuzingatia usawa kwa binaadamu.
Kiongozi Mwandamizi wa dhehebu la Kiislamu la Shia Ithnashery nchini Tanzania Imamu Swadiq Sheikh Hemed Jalala ameitaka Serikali ya awamu ya tano kuzingatia utawala bora na kuweka usawa baina ya wananchi bila ya kuangalia tofauti zao ili kwa pamoja waeze kujiletea maendeleo.
Sheikh Jalala ameitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mrithi wa Mtume Muhamad Imam Ali ambae alikufa miaka elfu moja na 30 iliyopita lakini anakumbukwa kwa utawala wake wa kuzingatia usawa kwa binaadamu.
Aidha Sheik Jalala amesema kuwa Utawala bora hauwezi kupatikana kama hakutakuwa na utulivu na amani katika nchi hivyo serikali ya awamu ya tano isimamie kikamilifu suala la amani na utulivu ili wananchi waweze kufanya kazi kwa bidii.

No comments:

Post a Comment