Monday 2 May 2016

Tazama jinsi Wakuu wa Idara zote za jiji la Dar es salaam wa kiapa kiapo cha kazi mbele ya Mkuu wa Mkoa Dar es salaam.

Wakuu wa Idara zote za jiji la dsm pamoja na maafisa Utumishi wa halmashauri za jiji wamesaini kiapo cha kazi mbele ya Mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya baada ya kubainika kutoa taarifa zisizo za kweli dhidi ya kuwepo kwa watumishi hewa katika idara zao baada ya kubainika watumishi hewa wengine 209 katika Uchunguzi wa Siku chache zilizopita.


Miongoni mwa masharti yaliokuwapo katika kiapo hicho ni kwamba iwapo ikigundulika  kuwapo kwa watumishi hewa katika idara husika baada wiki moja  ijayo,Afisa utumishi au mkuu wa idara hiyo atalipa gharama za mishahara iliyopotea,kushitakiwa kwa uhujumu uchumi,kuachishwa kazi lakini pia kufikishwa mahakamani.

Hatua ya kusaini na kula kiapo inatokana na baadhi ya wakuu wa idara pamoja na maafisa Utumishi katika jiji la DSM  kudaiwa kutoa taarifa za uongo kwa Mkuu wa mkoa Paul Makonda na wakuu wa wilaya za jiji hilo baada ya kutoa  idadi ndogo ya watumishi hewa kwa  mkoa wa dsm ambao walikuwa 74 tu, huku uhakiki wa sasa uliofanywa na tume maalum ukibaini  watumishi hewa 209 ambao wametafuna kiasi cha takribani shilingi bilion 2.7

Kiapo hicho cha kazi kiliionekana kuwa mwiba kwa watumishi hao wa mkoa wa DSM  kutokana na wengi wao kushindwa kujaza,huku wakileta hoja ambazo zilionekana kutokuwa na nguvu kwa mkuu wa mkoa kwa kuogopa kujifunga mpaka pale Bwana Makonda alipotoa dakika 5 kujaza na kuwasilisha.

Baadhi ya wakuu wa idara pamoja na maafisa utumishi wamesema kiapo hicho ni kizuri kwa ajili ya Utendaji kazi lakini ni mwiba kwa wakuu wa idara hasa kutokana na wengi wao kufanya kazi kwa mazoea, huku Katibu tawala wa mkoa wa Dsm THERESIA MBANDO akikiri kuwepo kwa taarifa zenye utata juu ya idadi ya watumishi hewa

No comments:

Post a Comment