Friday 18 December 2015

Profesa sospita muhongo amefanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha kuzalishia umeme cha mbezi power plant jijini Dar es salaam.



Waziri wa nishati na madini Profesa Sospita Muhongo pichani  leo  amefanya ziara ya kushtukiza katika  kituo cha kuzalishia umeme cha  mbezi power plant  jijini Dar es salaam.
Akizungumza na meneja  uzalishaji injinia Mohammed Kisiwa lengo la kufanya ziara  hiyo  ni kutokana na wananchi kulalamikia suala la bei ya umeme kuwa juu pamoja na kukatika mara kwa mara.
 Waziri muhongo  amesema katika kuzipatia ufumbuzi kero hizo kesho anatarajia kukutana na viongozi wa tanesco ili majibu yaweze kupatikana.
 Hivi karibuni baadhi ya mawaziri wamekuwa wakifanya ziara za kushitukiza ikiwa ni katika kutimiza dhana ya uwajibikaji na kauli mbiu ya mh,Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania dk John Pombe magufuli ya HAPA KAZI TU.

No comments:

Post a Comment